Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Craig Burley: Haaland usiposhinda Ballon d'Or usirudi tena

Haaland Craig Burley Craig Burley na Haaland.

Thu, 14 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mchambuzi wa michezo na mchezaji wa zamani wa Chelsea, Craig Burley amemwambia Haaland kwamba ikiwa hatashinda tuzo ya Ballon d'Or mwaka huu basi asirudi tena kushiriki kwenye sherehe za tuzo hiyo.

"Lionel Messi ameshinda Kombe la Dunia na ni mafanikio makubwa, lakini ni kipindi cha wiki nne. Fomu yake ya jumla ya ubingwa haikuwa bora zaidi.

"PSG wamekuwa wabaya, Erling Haaland… mabao 50+, taji la Ligi Kuu, Kombe la FA na Ligi ya Mabingwa. Erling anapaswa kushinda tuzo hii; Najua watu wengi hawawezi kuondoka kwenye treni ya Messi. Lakini angalia picha kubwa.

"Bei hii inanitia mashaka. Nadhani kutakuwa na rundo la hadithi za hisia. ‘Messi ameshinda Kombe la Dunia’, ‘Messi ndiye huyu.. na ‘Messi ni yule...’ na watampa nyingine.

"Kama ningekuwa Erling Haaland, nisingerudi tena kwenye sherehe ya Ballon d'Or maishani mwangu kama hangeshinda mwaka huu, kama Robert Lewandowski," amesema Craig Burley.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: