Timu za Taifa za Afrika Kusini na Congo DR, kila mmoja ataondoka na kitita cha Tsh bilioni 6.3 baada ya kushika nafasi ya tatu na ya nne kunako michuano ya AFCON 2023 pale Ivory Coast.
Ikumbukwe kuwa, Afrika Kusini imemaliza michuano ya AFCON 2023 katika nafasi ya tatu wakati Congo DR ikimaliza nafasi ya nne.
Afrika Kusini watapata faida ya kuondoka na medali ya shaba na pesa Tsh bilioni 6.3 wakati wazee wa mtaa wa nne Congo DR wataondoka na mpunga wao Tsh bilioni 6.3 kimya kimya kwenda kula bata.
Kwa upande wa Afrika Kusini wao, Tsh bilioni 6.3 watagawana wachezaji na benchi lao la ufundi hapa Chama Cha Soka hakipati chochote.