Klabu ya Coastal Union inayoshiriki Ligi kuu kandanda Tanzania Bara kutoka Jijini Tanga, imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Yanga Fiston Abdulrazack raia wa Burundi.
Klabu ya Coastal Union inayoshiriki Ligi kuu kandanda Tanzania Bara kutoka Jijini Tanga, imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Yanga Fiston Abdulrazack raia wa Burundi. Fiston aliwahi kucheza kwenye klabu ya Yanga kwa nusu msimu na baada ya kutokufanya vyema akaondoshwa klabuni hapo. Huu ni usajili wa kuongeza nguvu kwenye kikosi cha Coastal Union baada ya kuondokewa na baadhi ya wachezaji wake msimu huu.