Sat, 21 May 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Coastal Union wameibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Dodoma Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara mchezo uliopigwa jana Ijumaa katika Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Mabao ya Coastal yamefungwa na Abdul Suleiman ‘Sopu’ yote mawili dakika ya saba na 15, wakati la Dodoma Jiji limefungwa na Anuary Jabir dakika ya 23.
Coastal Union wanafikisha pointi 31 na kusogea nafasi ya tisa, huku Dodoma Jiji ikibaki na pointi zake 28 nafasi ya 11 baada ya wote kucheza mechi 25
Chanzo: www.tanzaniaweb.live