Tue, 6 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Wagosi wa Kaya, Coastal Union imesema imejianda kuwashangaza walima Alizeti, Singida Big Stars Katika Mchezo ambao utachezwa kesho katika Uwanja wa Liti Mkoani Singida.
Kocha wa Timu hiyo Chippo Yusuph, baada ya Kuboronga Katika Mchezo kadhaa ya Ligi kuu Mpango wao ni Kuzindukia Katika Mchezo wa Kesho kwa Kuvuna Alama Tatu na Kuendelea Kutembeza Kichapo wa Wapinzani wengine walio Mbele yao.
Nahodha wa Wagosi hao wa Kaya, Jackson Salvatory amewatoa hofu Mashabiki wa Timu kuwa kamwe Timu hiyo haitashuka Daraja kwa Sababu Siku za Furaha kwa Mashabiki wa Timu Hiyo Zimewadia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live