Fri, 1 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Coastal Union wamefanikiwa kuchukua alama zote tatu dhidi ya Geita FC kwenye uwanja wao wa nyumbani CCM Mkwakwani jijini Tanga.
Coastal wamewafunga Geita goli 3-1 jana Novemba 30, 2023 ambapo magoli yao yalifungwa na Roland Beakou dakika 30, Maabad Maulid '53' na Semfuko Charles dakika ya 59.
Goli pekee la kufutia machozi la Geita lilifungwa na Valentino Mashaka dakika 12 ya mchezo.
Coastal Union wamefikisha alama 13 kwenye msimamo wakiwa nafasi ya 9 huku Geita wakiwa nafasi ya 10 na alama zao 13 wakitofautiana kwa magoli ya kufunga na kufungwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live