Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Coastal Union maji ya shingo, watepeta kwa Geita Gold

Gita Vs Coastal Nyankumbu.jpeg Geita wameibuka na ushindi wa bao 1-0

Tue, 24 Jan 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Timu ya Geita Gold imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Nyankumbu mjini Geita.

Bao pekee la Geita Gold limefungwa na Edmund John dakika ya 17 na kwa ushindi huo wanafikisha pointi 31 katika mchezo wa 22, ingawa wanabaki nafasi ya tano wakizidiwa pointi 12 na Singida Big Stars ambao wamecheza mechi 21.

Kwa upande wao Coastal Union baada ya kichapo cha leo wanabaki na pointi zao 19 za mechi 22 nafasi ya 13.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live