Shirikisho la soka nchini Misri limetangaza kujiuzulu kwa mwamuzi wa zamani wa EPL, Mark Clattenburg katika nafasi ya Rais wa kamati ya waamuzi nchini humo usiku wa kuamkia Alhamisi Januari 26, 2023 sababu ikitajwa kuwa kukosolewa na Rais wa klabu ya Zamalek, Mortada Mansour.
Bodi ya wakurugenzi ya Chama cha Soka cha Misri iliamua, katika mkutano wake wa dharura jana kukubali kujiuzulu kwa Mark Clattenburg,” EFA iliandika pia kwenye Twitter.
Clattenburg wiki hii alikosolewa na rais wa klabu ya Zamalek, Mortada Mansour, kwenye chaneli ya runinga ya Zamalek. Clattenburg alipandishwa cheo na kuwa mwamuzi wa mechi za Ligi Kuu England mwaka 2004 baada ya misimu mitatu katika ligi hiyo.