Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Cissé kuongezwa Mkataba Senegal

Aliou Cisse 1140x640 Aliou Cissé

Thu, 18 Jul 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Shirikisho la soka la Senegal (FSF) linataka kumuongeza mkataba Kocha Aliou Cissé hadi fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 nchini Morocco.

Cissé ambaye amekuwa ofisini tangu Machi 2015, ndiye Kocha aliyekaa muda mrefu zaidi katika historia ya Senegal. Mkataba wake wa sasa unamalizika mwishoni mwa Agosti.

Licha ya kuondolewa kwa Senegal katika hatua ya 16 ya AFCON 2023, Rais wa FSF, Augustin Senghor, alisisitiza imani yake kwa Cissé .

Ikiwa Cissé ataongeza mkataba wake, atapata fursa ya kucheza AFCON yake ya 5 kama kocha wa Senegal. Pia atalenga kushinda AFCON yake ya pili akiwa na timu ya taifa baada ya ushindi wao mwaka wa 2021.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live