Tue, 3 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Beki wa Chelsea na timu ya Uingereza Ben Chilwell atakuwa nje ya uwanja kwa takribani miezi miwili ijayo kufuatia majeraha mapya aliyoyapata wiki iliyoisha!
Ben anatarajiwa kurejea uwanjani baada ya miezi miwili kupita japo itategemea na kasi ya kupona kwake inaweza pia kuwa zaidi ya miezi miwili!
Michezo ambayo mwingereza anaweza kucheza ni ile ya karibu na Christmas kutokana na taarifa za ndani ya klabu ya chelsea zinavyoeleza.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live