Chelsea imeibuka na ushindi wa bao 2-0 dhidi ya AC Milan katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya huku mlinzi wa zamani wa Chelsea Fikayo Tomori akionyeshwa kadi nyekundu ya mapema kabisa.
Tomori alimvuta jezi kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa England Mason Mount kabla ya refarii Daniel Siebert kuamua kuwa tuta na kadi nyekundu, tuta ambalo likafungwa na kiungo mkabaji wa Italia Jorginho kabla ya bao la Pierre-Emerick Aubameyang kufunga bao la pili kwenye mchezo huo
Ushindi wa Chelsea unaendeleza wigo wa ushindi kwa kocha mpya wa klabu hiyo Graham Potter sasa anafikisha mechi tano bila kupoteza.
Chelsea inaongoza kundi ikifuatiwa na RB Salzburg ambayo ilitoka sare ya bao moja kwa moja na Dinamo Zagreb