Tue, 7 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msenegal Nicholas Jackson amefunga hat-trick Chelsea ikiibamiza Tottenham Hotspur jumla ya magoli 4-1 kwenye Derby ya Jiji la London.
Magoli ya Chelsea katika mchezo wa jana yamefungwa na Palmer (P) 35' na Jackson 75' 90+4' 90+7' huku goli pekee la Spurs likifungwa na Kulusevski 6'.
Spurs imepoteza mechi yake ya kwanza ya msimu baada ya kulazimika kumaliza ikiwa pungufu ya wachezaji wawili baada ya Christian Romero na Destiny Udogie kuoneshwa kadi nyekundu.
Mauricio Pochettino ameiongoza Chelsea kuwaadhibu Waajiri wake wa zamani katika dimba la Tottenham Hotspur.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live