Mon, 3 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkufunzi Enzo Maresca amesaini mkataba wa miaka mitano ya kuitumikia Chelsea kama kocha mkuu akichukua mikoba ya Mauricio Pochettino aliyetupiwa virago.
Maresca (44) raia wa Italia anatua klabuni hapo kwa mkataba mpaka Juni 2029 wenye chaguo la kuongezeka mpaka Juni 2030 baada ya kuipandisha daraja Leicester City.
Chelsea itailipa Leicester City fidia ya Euro milioni 10 kwa ajili ya kocha huyo pamoja na wasaidizi wake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live