Tue, 12 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Chelsea Football Club iliulizia uwezekano wa kuipata saini ya mshambuliaji wa Nottingham Forest, Taiwo Awoniyi raia wa Nigeria masaa 48 kabla ya dirisha la usajili kufungwa lakini Nottingham wakakataa ofa hiyo.
Siku moja baada ya dirisha la usajili kufungwa Nottingham Forest wakakutana na Chelsea katika ushindi wa goli 1-0 huku Awoniyi akitoa pasi ya usaidizi wa goli.
Na sasa ametajwa miongoni mwa wale wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa mwezi wa Ligi kuu soka England.
Chelsea kwa sasa inakabiliwa na idadi kubwa ya majeruhi huku mwamba huyo akiendelea kupeta EPL.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live