Klabu ya Chelsea haijakata tamaa juu ya mpango wa kuinasa saini ya kiungo wa Benfica na Timu ya Taifa Argentina Enzo Jeremias Fernandez licha ya jaribio la awali kukataliwa mwanzoni mwa mwezi huu.
Klabu ya Chelsea haijakata tamaa juu ya mpango wa kuinasa saini ya kiungo wa Benfica na Timu ya Taifa Argentina Enzo Jeremias Fernandez licha ya jaribio la awali kukataliwa mwanzoni mwa mwezi huu. Awali The Blues walitaka kutoa zaidi ya thamani ya kifungu cha kuachiwa cha pauni milioni 106 kwa awamu tatu (pauni milioni 37.3 kwa kila awamu) kukwepa vikwazo vya sheria ya matumizi ya kiungwana na fedha (FFP) lakini miamba hiyo ya Ureno inataka pesa hizo zilipwe kwa pamoja.