Wenyeji Chelsea wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya AFC Bournemouth katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa jana Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
Wenyeji Chelsea wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya AFC Bournemouth katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa jana Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London. Mabao ya The Blues katika mchezo huo yamefungwa na Kai Havertz dakika ya 16 na Mason Mount dakika ya 24 na kwa ushindi huo wanafikisha pointi 24 katika mchezo wa 15 na kusogea nafasi ya nane, wakati AFC Bournemouth inabaki na pointi zake 16 za mechi 16 nafasi ya 14.