Thu, 5 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mazungumzo ya Chelsea na Benfica juu ya kumsajili Enzo Fernandez yamekwama baada ya vilabu hivyo kushindwa kupatana juu ya mfumo wa malipo ya ada ya Euro milioni 85.
Chelsea kamwe haikujadili kifungu cha kuachiwa cha Euro milioni 120. Benfica sasa inataka kiasi hicho kilipwe.
Enzo amekuwa akiwindwa na vilabu vingi Barani Ulaya baada ya kumalizika kwa michuano ya Kombe la Dunia huku akibeba taji hilo na kuchaguliwa kuwa mchezaji bora chipukizi wa michuano hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live