Thu, 7 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mashetani Wekundu, Manchester United wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi yanChelsea katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa kusmkia leo Uwanja wa Old Trafford Jijini Manchester.
Mabao yote ya Mashetani Wekundu yamefungwa na Scott McTominay dakika ya 19 na 69, wakati bao pekee la The Blues limefungwa na Cole Palmer dakika ya 45.
Kwa ushindi huo, Manchester United inafikisha pointi 27 na kusogea nafasi ya sita, wakati Chelsea inabaki na pointi zake 19 nafasi ya 10 baada ya wote kucheza mechi 15.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live