Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Chelsea mdomoni mwa wakali wapya wa EPL

New Castle Vs Chelsea Chelsea watakuwa ugenini dhidi ya Newcastle

Sat, 12 Nov 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Chelsea ambayo ipo chini ya kocha mkuu Graham Potter watakuwa ugenini hii leo kukipiga dhidi ya Newcastle United baada ya kushindwa kupata matokeo katika mechi nne mfululizo.

Mechi ya mwisho ya Chelsea ametoka kupoteza kwenye mchezo wake wa Dabi ya London walipokuwa wakicheza dhidi ya The Gunners huku Matajiri wapya wa Uingereza wakiwa wametoka kushinda mechi iliyopita.

The Blues wamekuwa wakipitia wakati mgumu baada ya kupata majeraha ya wachezaji wake akiwemo Recce James, Fofana na Chilwell ambao hao wote ni mabeki ambao kwa asilimia kubwa wanaanza kwenye kikosi cha kwanza.

Baada ya kucheza michezo 13 amejipatia pointi 21 huku akiwa amepoteza mechi nne, na anazidiwa pointi 13 na kinara wa Ligi Arsenal ambaye ana pointi 34 baada ya kupoteza mechi yake moja.

Wakati huo huo Newcastle United wao wapo nafasi ya 3, wakiwa na pointi 27 baada ya kucheza michezo 14 kwenye Ligi huku mechi ya mwisho kukutana timu hizi mbili Chelsea alishinda.

Kocha wa Newcastle Eddie Howe akichukua tuzo ya kocha bora wa mwezi Oktoba, huku mchezaji wa timu hiyo Miguel Almiron akichukua tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Oktoba kutokana na kiwango alichokionyesha.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live