Thu, 16 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha mkuu wa kikosi cha Chelsea Mauricio Pochettino hana mpango wa kuondoka Chelsea mwisho wa msimu huu na tayari ameanza zoezi la kuwafuatilia nyota watakaojiunga na kikosi hicho msimu ujao.
Miongoni mwa nyota walio kwenye mipango ya kocha huyo ni mshambuliaji wa SSC Napoli Victor Osimhen japo matumaini yameanza kuwa madogo ya kuinasa saini ya nyota huyo kutokana na nafasi iliyopo hivi sasa Chelsea.
Klabu ya Arsenal pia imeingiza mkono wake kwa ajili ya kuinasa saini ya Osimhen na ina nafasi kubwa kutokana na ushiriki wake wa UEFA msimu ujao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live