Fri, 31 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya soka ya Chelsea imetangaza kuwa jezi zilizovaliwa na wachezaji katika mchezo wao dhidi ya Everton Machi 18, 2023 zitapigwa mnada ili kupata fedha za kugharamia, ukamilishaji wa shule ambayo marehemu Christian Atsu alikuwa akiijenga nchini Ghana.
Christian Atsu ni nyota aliepita katika klabu ya Chelsea na alifariki katika tetemeko la Ardhi lililotokea nchini Uturuki.
Mchezo huo ulimalizika kwa sare ya magoli 2-2.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live