Thu, 2 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Vinara kunako EPL, Chelsea jana wameibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya wenyeji, Watford katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Vicarage Road mjini Watford.
Mabao ya Chelsea yalifungwa na Mason Mount dakika ya 29 na Hakim Ziyech dakika ya 72, wakati la Watford lilifungwa na Emmanuel Dennis 43.
Chelsea inafikisha pointi 33 na kuendelea kuongoza Ligi kwa pointi moja zaidi ya Manchester City na mbili zaidi ya Liverpool baada ya timu zote kucheza mechi 14, wakati Watford inabaki na pointi zake 13 za mechi 14 nafasi ya 17.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live