Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Chelsea Wataka FA Cup Kuchezwa Bila ya Mashabiki

Helesea The Blues Chelsea Wataka FA Cup Kuchezwa Bila ya Mashabiki

Tue, 15 Mar 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Chelsea wamekitaka chama cha soka nchini Uingereza FA kurusu mchezo wa robo fainali dhidi ya Middlesbrough kuchezwa bila ya mashabiki ili kuleta usawa wa kimechezo kutokana na wao kuzuiwa kuuza tiketi kwa mashabiki wao na wageni.

Chelsea kwa sasa inaendeshwa kwa kibali maalumu ili kuweza kumalizia michezo inayowakabili kwenye msimu huu na kuweza kulipa wafanyakazi baada ya miliki wa klabu hiyo kuwekezea vikwazo huku mali zake zikishikiliwa na serikalia ya Uingereza.

“Tunasikitika kutangaza kuwa hatutaweza kuuza tiketi kwenye mchezo wa FA Cup jumamosi dhidi ya Middlesbrough,” waraka wa Chelsea ulisema.

“Japokuwa tumekuwa na mazungumzo ya kina na ofisi ya vikwazo vya kifedha na utekelezaji (OFSI) tarehe ya mwisho wa uuzaji wa tiketi za ugenini zimepita pasipo marekebiso sahihi kufanya na serikali kwenye kibali ambacho kingeruhusu uhudhuriaji wa mashabiki wa Chelsea viwanjani.

“Chelsea FC inatambua madhara ya makubwa yatakayowapata Middlesbrough na mashabiki wake, pia mashabiki wetu ambao tayari wamenunua tiketi kabla ya kabla ya katazo, lakini tunaamini hii ni haki kwa ajiri ya pande zote mbili kutokana na hali ilivyo sasa.

“Tutaendelea kufanya mazungumzo kwa ajiri ya uuzaji wa tiketi na OFSI knyenye michezo mingine ambayo bado tunacheza na tuna tumai kupata muafaka.”

FA walijibu kwa waraka mfupi ambao ulisomeka: “Tunatambua maombi ya chelsea kucheza kwenye mchezo wa robo fainali ya FA Cup dhidi ya Middlesbrough kucheza pasipo, swala hili litajadiliwa kwenye kikao cha Professional Game Board siku ya jumatano.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live