Mon, 27 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchambuzi wa soka Bongo, George Ambangile amesema bado yupo njia panda, anahoji je! Kwenye Mechi kati ya Simba dhidi ya Asec Mimosas, Che Malone alikuwa anacheza namba ngapi?
Akiuzungumzia mchezo huo, Ambangile alisema, alipokuwa anautazama ilibidi naye awe anawauliza wenzake sababu hakuwa akielewa kilichokuwa kinaendelea na kumsababishia kazi kubwa sana beki wa kati wa Simba, Henock Inonga.
"Nilikuwa sielewi maana kuna kuwakati unamuona namba sita, mara kapanda juu kwenye nafasi ya namba kumi au nane, hakuwa akieleweka. Kuna wakati nilikuwa namuonea tu huruma Inonga," alisema Ambangile.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live