Wed, 3 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo mpya wa Yanga SC, Clatous Chota Chama ameiaga familia ya Wanasimba huku akikumbuka namna alivyotua ndani ya timu hiyo akiwa hafahamiki na baadae kuwa vile ambavyo wapenda soka wanamfahamu.
“Sina chochote zaidi ya heshima kwa kila mmoja wenu kwa upendo na heshima ambayo mmenipa miaka yote hii na hakuna yeyote anayeweza kubadilisha historia tuliyoitengeneza pamoja,” sehemu maneno ambayo ameyaandika Chama akiwaaga mashabiki wa Simba.
Kwa sasa nyota huyo raia wa Zambia ametua Yanga, akitangazwa asubuhi ya Julai 1, 2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live