Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Cedric Kaze: Tumejitafuta, tumejipata

Image 120 1140x640.png Cedric Kaze: Tumejitafuta, tumejipata

Sun, 10 Sep 2023 Chanzo: Dar24

Baada ya kuanza vibaya kwenye michezo yao miwili ya kwanza ya Ligi Kuu Tanzania Bara, Kocha Mkuu wa kikosi cha Namungo FC, Cedric Kaze ameweka wazi kuwa tayari wameona wapi walikuwa wanakosea na kuahidi kufanya makubwa kwenye michezo yao ijayo.

Kocha huyo kutoka nchini Burundi ameweka wazi kuwa anajivunia namna ambavyo wachezaji wake wamekuwa wakitimiza maelekezo ya Program anazotoa.

Kaze amesema: Nafurahishwa na namna ambavyo tumekuwa na maendeleo mazuri ya Programu za maandalizi ya michezo yetu ijayo hasa kutokana na kuanza ligi kwa kusuasua.

Tumerekebisha makosa yetu na sasa ni muhimu kuendelea na kasi hii kwa ajili ya mechi zijazo kwani ushindani ni mkubwa na kila timu inahitaji matokeo.”

Chanzo: Dar24
Related Articles: