Tue, 7 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkufunzi wa zamani wa timu ya Taifa Misri na Africa Kusini (Bafana Bafana), Carlos Queiroz ameteuliwa kuwa kocha mkuu wa timu ya Taifa Qatar.
Queiroz ambaye amewahi kuhudumu kama kocha msaidizi wa Sir Alex Ferguson kunako Manchester United alikuwa kocha wa Iran kwenye michuano ya kombe la Dunia 2022.
Queiroz (69) raia wa Ureno pia amewahi kuwa kocha klabu ya Real Madrid, timu za Taifa Ureno, Colombia na Saudi Arabia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live