Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Carabao: Newcastle yailaza Manchester City

Carabao: Newcastle Yailaza Manchester City Carabao: Newcastle yailaza Manchester City

Thu, 28 Sep 2023 Chanzo: Bbc

Mkufunzi wa Newcastle Eddie Howe anasema timu yake ina hamu ya "kupanda nafasi moja bora" kuliko washindi wa pili wa msimu uliopita wa Kombe la Carabao baada ya timu yake kuishinda Manchester City na kufika raundi ya nne ya kampeni hii.

Alexander Isak alifunga bao la ushindi kwa kikosi cha pili cha Newcastle, ambao walipata uhai baada ya mapumziko na kuwashinda City ambao walikuwa wamebadilika kikosi chao.

Newcastle, ambao walipoteza kwa Manchester United katika fainali mwaka jana, walifanya mabadiliko 10 kutoka kwa ushindi wa 8-0 Jumapili dhidi ya Sheffield United na hawakupata kiki katika kipindi cha kwanza kilichotawaliwa na wageni.

Lakini baada ya Bruno Guimaraes na Anthony Gordon kuingia baada ya mapumziko, Magpies ilibadilika, na Isak akifunga bao kufuatia kazi nzuri kutoka kwa Joelinton.

"Tunataka kujaribu na kwenda mbele zaidi kama tunaweza lakini kuna safari ndefu katika hatua hii. Bado tuko pale tunapambana.

"Wakiwa na nidhamu lakini wazembe mbele ya utawala wa City wa kumiliki mpira, vijana wa Howe walikuwa na bahati ya kusawazisha baada ya dakika 45, huku Julian Alvarez akikosa nafasi mbili nzuri.

Pep Guardiola alifanya mabadiliko saba, akimpatia fursa ya kwanza kiungo chipukizi Oscar Bobb miongoni mwao.

Lakini wenyeji walistahili ushindi wao kutokana na mchezo mzuri katika kipindi cha pili.Kwa Guardiola mechi hiyo ilikuwa ya pili katika mechi 38 kwa klabu yake kulazwa katika michuano yote.

Matokeo Mengine

Aston Villa 1. Everton 2

Blackburn 5 Cardiff 2

Bournemouth 2 Stoke 0

Brentford 0 Arsenal 1

Chelsea 1 Brighton 0

Liverpool 3 Leicester 1

Chanzo: Bbc