Wed, 25 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kesi inayomuhusu Mshambuliaji wa Simba Bernard morrison na Klabu ya Yanga mpaka sasa bado giza kutokana na mahakama ya usuluhishi ya masuala ya kimichezo CAS kutotoa maamuzi yoyote yale.
Kwa mujubu wa CAS kesi hiyo ingetolewa hukumu siku ya jana Agosti 24 na si zaidi ya hapo lakini mpaka kufikia majira ya saa sita za usiku bado hakukua na taarifa zozote kuhusu kesi hiyo.
Klabu ya Yanga ilipeleka shauri lake kwa mahakama hiyo wakimlalamikia Morrison kuvunja mkataba halali na kujiunga na mahasimu wao Simba SC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live