Fri, 12 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemkumbuka nahodha wa kikosi cha timu ya Taifa Tanzania ‘Taifa Stars’ Mbwana Samatta kwa kuchapisha picha yake katika ukurasa rasmi wa CAF.
Picha ya Samatta anayekipiga PAOK ya nchini Ugiriki imewekwa katika ukurasa huo na kuandikia maneno mfungaji mabao, mnyanyua mataji na muweka historia.
Ndani ya Afrika nyota huyo aling’aa na klabu ya TP Mazembe ya nchini Congo na amewahi kushinda nayo mataji mbalimbali ya Afrika na makombe ya ndani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live