Kikosi cha Burnley kimefanikiwa kurejea kwenye Ligi Kuu England ikiwa ni mara ya kwanza tangia washuke daraja msimu uliopita.
Kikosi hicho kimepanda daraja chini ya uongozi wa kocha na mchezaji wa zamani wa Manchester City Vincent Kompany, hiyo ni baada ya kupata ushindi dhidi ya Middlesbrough ambayo inashika nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi daraja la kwanza.
Mpaka sasa, The Clarets ambao hawajafungwa msimu huu, walifunga magoli yake kupitia kwa Ashley Barnes na Connor Roberts bao la kufutia machozi la Middlesbrough limefungwa na Chuba Akpom.
Matokeo hayo yanaifanya Burnley kuwa kileleni mwa msimamo wa Ligi hiyo kwa tofauti ya pointi 19 dhidi ya timu iliyonafasi ya pili Sheffield United, Luton mechi zikibakia sita.