Tue, 2 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Azam FC, Bruno Ferry amechaguliwa kuwa Kocha Bora wa mwezi Machi wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/24 akiwashinda kocha wa Yanga, Miguel Gamondi na Kocha wa Mtibwa, Zubeir Katwila.
Bruno aliiongoza Azam kushinda michezo miwili kati ya mitatu iliyocheza na kuendelea kubaki nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Azam iliifunga Yanga mabao 2-1, iliifunga Dodoma Jiji mabao 4-1 kisha ikatoka sare ya bao moja na Coastal Union.
Pia Kamati ya Tuzo imemchagua Meneja wa Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma, Shabani Rajabu, kuwa Meneja Bora wa Uwanja kwa mwezi Machi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live