Thu, 15 Aug 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bruno Fernandes amesaini nyongeza ya mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia Manchester United mpaka Juni 30, 2027 wenye chaguo la kuongezeka kwa mwaka mmoja zaidi.
Bruno raia wa Ureno ambaye atatimiza umri wa miaka 30 mwezi ujao alijiunga na Mashetani hao Wekundu mnamo Januari 2020 na kuifungia klabu hiyo magoli 73 na ‘assists’ 65 kwenye zaidi ya mechi 220.
Bruno atakuwa mmoja wa wachezaji wanaolipwa mshahara mkubwa klabuni hapo sambamba na Marcus Rashford na Casemiro baada ya kuongeza mkataba mpya.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live