Mon, 18 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezaji nyota wa Manchester United, Bruno Fernandes amepata ajali ya gari majira ya asubuhi Jijini Manchester.
Taarifa zinaeleza kuwa wahusika wote katika ajali hiyo hakuna aliyepata majeraha mabaya katika ajali hiyo.
Fernandes anatarajiwa kufanya mazoezi na wachezaji wengine wa kikosi cha Ralf Rangnick leo, kabla ya kumenyana na Liverpool kwenye Ligi ya Uingereza Jumanne usiku.
Hata hivyo kwa upande wa klabu ya Manchester United hawajatoa taarifa yoyote mpaka wakati huu kuhusiana na ajali hiyo wala maendeleo ya mchezaji wake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live