Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bruno Fernandes akosolewa Man United

Bruno Fernandes X Marus Lost Fernandes akosolewa Man United

Mon, 18 Dec 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Tarehe 8 Septemba 1994 ni siku muhimu sana kwa kijana wa Kireno kutoka mitaa ya Maia, Bruno Miguel Borges Fernandes ni jina lililo kwenye vitabu vya kumbukumbu ya mashabiki wengi wa soka ikiwemo mashetani wekundu Utd.

Alianza safari yake ya soka kutoka mitaani klabu ya Infesta na baadaye alipata ofa ya kujiunga na Akademi ya Porto lakini alikataa na kujiunga na mahasimu wao klabu ya Boavista ambao walikuwa wakimpa pesa ya nauli kila siku alianza kucheza eneo la beki wa kati kabla yakusogezwa mbele na kuwa kiungo mshambuliaji.

Fernandes alikipiga sana huko ambapo alihamia Italia klabu ya Novara na alipewa majina kama “Maradona wa Novara” na Mini Rui Costa gwiji wa soka nchini Ureno.

Lakini unakumbuka tukio la Bruno na wenzake kujeruhiwa na mashabiki wapatao 50 wa Sporting Lisbon May 15, 2018 baada ya kumaliza nafasi ya tatu na kukosa michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, mara hii tena nahodha huyo amekutana na ukosoaji mkubwa kutoka kwa tajiri anayepewa nafasi ya umiliki wa kalbu ya Manchester United Sir Jim Ratcliffe.

Ratcliffe anatarajiwa kujiunga na United hivi karibuni baada ya kukubaliana kununua asilimia 25 ya hisa za klabu, na atapewa udhibiti wa shughuli za soka.

Ratcliffe amezindua kitabu chake kinachoelezea historia ya INEOS, kampuni yake ya kemikali aliyoianzisha miaka 25 iliyopita.

Wakati wa ufunguzi wa “Grit, Rigour & Humour: the Ineos Story,” Ratcliffe anakumbushia safari yake kwenda Pacific alivyoona “ardhi ikitetemeka kila wakati Mshambuliaji wa Kisiwa cha Cook alipogongana na mchezaji mwingine katika mchezo wa Rugby.

Ratcliffe alibainisha jinsi mchezaji mmoja alivyovunjika mguu, lakini ilikuwa tofauti sana kwa Bruno Fernandes alivyoshikilia uso wake katika kipigo cha hivi karibuni dhidi ya Liverpool.

Tukio ambalo Ratcliffe analirejelea ni uchezaji wa Bruno Fernandes wakati wa kichapo cha 7-0 cha Manchester United ugenini dhidi ya mahasimu wao wa muda mrefu Liverpool ambapo alianguka chini akidai kupigwa na kiwiko, ingawa picha za marejeo zilionyesha alikuwa amepata pigo dogo kifuani.

Fernandes alikosolewa sana si tu kwa utendaji wake katika kipigo hicho bali pia kwa kumtupa refa msaidizi katika hatua za mwisho za mchezo.

United hawatakuwa na Fernandes wakati wakisafiri kwenda Anfiled katika mchezo huu mgumu kwa timu zote mbili, hii ni baada ya kupata kadi yake ya tano ya manjano msimu huu wa Ligi Kuu katika kipigo cha 3-0 dhidi ya Bournemouth.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live