Klabu ya Young Africans imetangaza kuachana na aliyekuwa kiungo wake mkabaji, Zawadi Mauya ambaye hatakuwa sehemu ya kikosi cha Young Africans msimu ujao 2024-2025 baada ya mkataba wake kutamatika.
Klabu ya Young Africans imetangaza kuachana na aliyekuwa kiungo wake mkabaji, Zawadi Mauya ambaye hatakuwa sehemu ya kikosi cha Young Africans msimu ujao 2024-2025 baada ya mkataba wake kutamatika. Mauya mwenye umri wa miaka 37 ambaye amekuwa mchezaji wa Young Africans SC kwa kwa misimu minne, anaondoka akiwa amemaliza muda wake. Kiungo huyo alitua Young Africans mwanzoni mwa msimu wa 2020-2021 akitokea Kagera Sugar.