Tue, 15 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) limeahirisha droo ya hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika (Caf Champions Cup) na Kombe la Shirikisho Afrika (Caf ConfederationCup) iliyokuwa ifanyike kesho Jumatano, November 16/2022 Jijini Cairo nchini Misri.
Shirikisho hilo limeomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza na kuongeza kwamba tarehe nyingine na muda ambao droo hiyo itafanyika itatangazwa baadaye.
Viongozi mbalimbali tayari walikuwa wameshawasili nchini Misri kwa ajili ya kuwakilisha timu zao na kushuhudia droo hiyo akiwemo CEO wa Yanga, Andre Martine.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live