Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Brazil yaanza na sare Copa America

Brazillll.jpeg Brazil yaanza na sare Copa America

Tue, 25 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Michuano ya kombe la Mataifa ya Amerika ya Kusini, Copa America 2024 imeendelea usiku wa kuamkia leo Juni 25, 2024 ambapo katika mchezo uliomalizika alfajiri hii, timu ya Taifa ya Brazil imelazimishwa sare tasa dhidi ya Costa Rica katika mchezo wa raundi ya kwanza wa Kundi D uliopigwa katika dimba la SoFi Stadium (Inglewood, CA).

Sare hiyo inaifanya Costa Rica kuweka rekodi ya kuepuka kipigo dhidi ya Brazil kwa mara ya kwanza tangu 1959 kufuatia vipigo 10 mfululizo.

Katika mchezo wa mapema wa Kundi D, kiungo wa zamani wa Real Madrid, James Rodriguez ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mechi akitoa asisti mbili katika ushindi wa 2-1 wa Colombia dhidi ya Paraguay.

Mabao ya Colombia yametiwa kimiani na nyota wa Crystal Palace, beki Daniel Munoz na kiungo Jefferson Lerma huku bao la kufutia machozi la Paraguay likifungwa na winga wa Brighton, Julio Enciso.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live