Sun, 11 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya taifa ya Brazil imeondoka jana Qatar baada ya kutolewa na Croatia katika mashindano ya Kombe la Dunia 2022.
Pichani, Richarlison akiwa na uso uliojaa unyonge anaonekana akijiandaa kupanda bus pamoja na kikosi chao kuelekea Airport.
Brazil iliondolewa na Croatia juzi katika hatua ya robo fainali baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika dakika 120.
Baada ya hapo yalitengwa matuta ambapo Croatia walitinga nusu fainali kwa ushindi wa penati 4-2.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live