Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Brazil na Argentina washindwa katika mechi za kufuzu Kombe la Dunia

Brazil Na Argentina Washindwa Katika Mechi Za Kufuzu Kombe La Dunia.png Brazil na Argentina washindwa katika mechi za kufuzu Kombe la Dunia

Wed, 11 Sep 2024 Chanzo: Bbc

Brazil na Argentina zimeshindwa katika mechi zao za hivi karibuni za kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2026.

Brazil walichapwa 1-0 ugenini Paraguay, ikiwa ni kichapo cha nne katika mechi zao tano zilizopita za kufuzu Kombe la Dunia.

Kipa wa Liverpool Alisson, kiungo wa Newcastle Bruno Guimaraes na mchezaji wa West Ham Lucas Paqueta wote walianza kucheza wakati wa mechi hiyo.

Wachezaji watatu wa Real Madrid Rodrygo, Endrick na Vinicius Jr walianza kwa kuwa washambuliaji upande wa Brazil.

Mabingwa watetezi wa kombe la dunia Argentina walipoteza kwa mabao 2-1 wakiwa ugenini dhidi ya Colombia, huku kiungo wa zamani wa Real na Everton James Rodriguez akifunga bao la ushindi kwa mkwaju wa penalti.

Lionel Messi, ambaye sasa anachezea Inter Miami, hakuchezea Argentina.

Kiungo wa kati wa Manchester United Manuel Ugarte, ambaye alijiunga na klabu hiyo mwezi uliopita akitokea Paris St-Germain, alianza kwa Uruguay katika sare ya 0-0 ugenini dhidi ya Venezuela.

Huko Amerika Kusini, Argentina inasalia kileleni mwa jedwali la timu 10 kwa alama mbili. Brazil sasa wanashikilia nafasi ya tano.

Chanzo: Bbc