Wed, 1 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mmiliki wa klabu ya Sheffield Wednesday inayoshiriki daraja la pili nchini Uingereza, Dejphon Chansiri amewaomba mashabiki wa klabu hiyo kuichangia klabu kiasi cha paundi milioni 2 kwa ajili ya kulipa mishahara ya wachezaji pamoja na kukidhi mahitaji mengine ya klabu,
Mmiliki huyo alisema kuwa
"Ikiwa watu 20,000 watatoa kiasi cha paundi £100 basi itakuwa ni sawa na jumla ya paundi milioni 2, hivyo Kiasi hicho cha pesa kitatosha kugharamikia kila kitu"
Chanzo: www.tanzaniaweb.live