Fri, 24 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema anashukuru kwamba bora zile goli 5-1 dhidi ya Yanga alifungwa Aishi Manula.
Ahmed amesema, Aishi ni golikipa mzoefu ambaye ameweza kuhimiri zile presha za mashabiki na kurudi haraka mchezoni tofauti na magolikipa wengine walipo klabuni kwao.
"Angefungwa Ally Salim au Ayoub ingekuwa ngumu sana kwao kurudi mchezoni. Zile presha za kuambiwa umepanga matokeo, kusemwa vibaya mitandaoni ingewasumbua sana lakini kwa Aishi ni vitu vya kawaida," alisema Ahmed.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live