Wed, 1 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Simba Sports Club, Clatous Chama amefungiwa michezo mitatu (3) ya ligi na kutozwa faini ya Shilingi Milioni 1 (Tsh.1,000,000) kwa kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji Nickson Kibabage wa Yanga wakati wa mchezo wa Dabi ya Kariakoo.
Chama atakosekana katika michezo ambayo ni Simba dhidi ya Mtibwa, Tabora pamoja Azam FC.
Ni mara ya tatu kwa Chama kufanya kitendo kama kile. Aliwahi kumkanyaga kwa maksudi Fei Toto akiwa Yanga, Abal Kassim Suleiman wa Ruvu Shooting mwishoni mwa msimu uliopita na akafungiwa mechi za mwisho wa Ligi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live