Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imetangaza kuahirisha mchezo kati ya Simba SC dhidi ya Mtibwa Sugar uliopangwa kuchezwa Februari 18, 2024 katika dimba la Jamhuri Morogoro.
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imetangaza kuahirisha mchezo kati ya Simba SC dhidi ya Mtibwa Sugar uliopangwa kuchezwa Februari 18, 2024 katika dimba la Jamhuri Morogoro. Kwa mujibu wa taarifa ya TPLB, sababu za kuahirishwa kwa mchezo huo ni kutoa fursa kwa Simba SC, kujiandaa na safari yake ya kwenda Ivory Coast kuivaa Asec Mimosas kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) utakaopigwa Februari 23, 2024.