Kikosi cha Polisi Tanzania kimeanza vibaya katika Uwanja wa Ushirika uliokuwa umefungiwa kupisha marekebisho baada ya kukubali kichapo cha magoli 3-1 kutoka kwa Simba SC.
Katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya NBC ulishuhudia dakika za mwanzo za mchezo kila timu ikianza kwa kasi huku wakishambuliana kwa zamu.
Alikua ni John Bocco aliewatanguliza Simba kipindi cha kwanza akimaliza pasi safi ya Shomari kapombe kabla ya Phiri kuongeza bao la pili akitengenezewa na Clatous Chama.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika Simba walikua mbele kwa uongozi wa mabao 2-0.
Kipindi cha Pili Simba walirudi kwa kasi na kupata bao la tatu kupitia kwa Mzambia Moses Phiri na kuwanyong'onyeza wenyeji.
Dakika ya 90 Polisi Tanzania walipata bao la kufutia machozi na mpaka dakika 90 zinakamilika Simba wakafanikiwa kuondoka na alama tatu na kuwafanya wafikisha pointi 31 katika msimamo wa Ligi na kusogea mpaka nafasi ya pili.