Tue, 1 Sep 2020
Chanzo: mwanaspoti.co.tz
KOCHA Msaidizi wa Gwambina FC, Athuman Bilali 'Bilo' amesema kwa muda mfupi aliokaa na Mkurugenzi wa Ufundi, Mwinyi Zahera amepata vitu vingi sana kwenye ufundishaji wa mchezo wa soka kutoka kwake.
Kabla ya kutua Gwambina, Zahera alifundisha Yanga kisha kuachana na klabu hiyo na sasa msimu ujao ataonekana kwenye benchi la ufundi akiwa na timu hiyo iliyopanda daraja kushiriki Ligi Kuu msimu huu.
Bilo amesema Zahera ni bonge la kocha kwani tangu ameanza kufanya naye kazi amefaidika na mbinu mbalimbali za ufundishaji wa soka lake ambazo kwake zitamsaidia.
Chanzo: mwanaspoti.co.tz