Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Billnass kumlipia faini Ally Kamwe TFF

Kamwe Ms Billnass Billnass kumlipia faini Ally Kamwe TFF

Fri, 20 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Msanii wa muziki Bongo Fleva ambaye pia ni mfanyabiashara na shabiki kindakindaki wa Klabu ya Yanga, William Lyimo maarufu kama Billnass amesema atalipa faini ambayo Ofisa Habari wa Klabu hiyo, Ally Kamwe amepigwa na Bodi ya Ligi.

Kamwe amepigwa faini ya Tsh million moja na Kamati ya Bodi ya Ligi kwa madai ya kumdhalilisha mwamuzi, Tatu Maologo mtandaoni.

Kupitia mtandao wa Instagram baada ya mchezo wa Ligi Kuu kati ya Singida FG FC na Simba Sc ambapo Simba ilishinda kwa bao 2-1, Kamwe alipost picha ya mwamuzi Tatu Malogo kisha akaiwekea wimbo wa Billnass uitwao 'Maokoto' jambo lililotafsriwa kuwa mwamuzi huyo kuhusishwa na kupokea rushwa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Billnass ameandika; "Pole sana (Ally Kamwe). Ila sisi kama Nenga Tronics kwa kidogo tulichojaaliwa tunaomba tumalize sisi (faini) japo tunajua (faini) iko ndani ya uwezo wako. Lakini najua MAOKOTO ni wimbo wako pendwa," amesema Billnass.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: