Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bilionea wa Yanga amshusha Msauzi, aanza na Morrison

94447 Mzauzi+pic Bilionea wa Yanga amshusha Msauzi, aanza na Morrison

Wed, 5 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

YANGA wanagawa dozi huku wakisema timu yao inaendeshwa kisasa na habari mpya ni kwamba kuna mtaalamu mwingine ameshushwa kimyakimya na ameanza kazi na mshambuliaji, Bernard Morrison.

Wadhamini wa Yanga ambao ni Kamapuni ya GSM inayomilikiwa na Biilionea, Ghalib Mohamed ndio waliosimamia pia usajili wa timu hiyo, sasa wanasuka benchi la ufundi na juzi Jumapili wakamshusha mtaalamu wa tiba za viungo, Faried Cassiem.

Cassiem alitua juzi usiku na jana Jumatatu haraka alianza kazi katika kuwatibu wachezaji wa timu hiyo ambao ni majeruhi.

Akiwa mazoezini jana na kushuhudiwa na Mwanaspoti, Cassiem raia wa Afrika Kusini alianza kazi kwa kuangalia majeraha ya Morrison ambaye alikuwa akilalamika maumivu baada ya kumalizika kwa mechi ya juzi dhidi ya Mtibwa Sugar.

Ujio wa Cassiem ni hatua ya kuyafanyia kazi mapendekezo ya kocha wao mpya, Luc Eymael ambaye alihitaji kuletewa mtu wa taaluma hiyo.

Mkurugenzi wa Uwekezaji wa GSM, Mhandisi Hersi Said ameliambia Mwanaspoti kwamba kampuni yao bado inahitaji kuiona Yanga inabadilika na kuendeshwa kisasa na ujio wa Cassiem ni uthibitisho mwingine wa kukamilisha dhamira yao wakishirikiana na uongozi wa Yanga.

Pia Soma

Advertisement
Hersi alisema tayari Cassiem ambaye alifanya kazi katika klabu mbalimbali za Afrika Kusini amemalizana na uongozi wao na sasa anaungana na Eymael katika kuboresha benchi la ufundi la timu hiyo.

“Kuna mambo lazima yaendeshwe kwa utaalamu hasa suala la matibabu, nikweli tumemleta Cassiem ambaye ni mtaalamu wa tiba za viungo hatua hii ni sisi GSM tukishirikiana na uongozi wa klabu ya Yanga kutekeleza mahitaji ya kocha mkuu,” alisema Said ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya mashindano ya timu hiyo.

Kabla ya kuja Yanga, Cassiem amefanya kazi katika klabu mbalimbali za Ligi Kuu Afrika Kusini zikiwemo Mamelodi Sundowns, Chips United na Ajax Capetown. Kwa kufanya hivyo, Yanga inaendana na falisafa za kuendesha klabu hiyo kisasa kama alivyotaka kocha wao mkuu.

Chanzo: mwananchi.co.tz