Jumla ya Tsh. 31,329,180,963.16 zitatumika kwa ajili ya ukarabati wa Uwanja wa Michezo wa Benjamin Mkapa kwa awamu ya kwanza ambapo hadi kufikia Aprili 2024 Tsh. Bilioni. 7.44 zimelipwa kwa Mkandarasi
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kupitia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, ukarabati huo unajumuisha Vyumba vya Wachezaji, Waandishi wa Habari, Watu Mashuhuri, Taa na Eneo la Kuchezea pamoja na Matangazo ya Kidigitali
Aidha, Wizara imesema awamu ya kwanza ya ukarabati katika maeneo mbalimbali katika Uwanja huo imefikia wastani wa kati ya Wastani wa 60%, 80%, 98% na maeneo mengine yamekamilika kwa 100%