Mon, 6 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezo wa fainali ya County kati ya Lofa County dhidi ya Ribergee County uligubikwa na ugomvi mkali uliosababisha mchezo kusimama kwa muda baada ya mchezaji wa Lofa kuchukua Biblia ya kipa wa River Gee na kuitupa wakati mechi ikiendelea.
Tukio hilo limetokea jana, Mei 5 huko Liberia katika mechi ya fainali za michuano ya Liberian National County Meet dakika ya 114 kwenye muda wa ziada wakati timu zote zikiwa zimefungana bao 2-2.
River Gee walishinda ubingwa wa kaunti kwa penati 3-1 dhidi ya Lofa, na hii ilikuwa mara yao ya kwanza kushinda taji hilo baada ya miaka 15.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live